HABARI MPENZI MWANAMICHEZO KARIBU KATIKA KURASA HII MAHSUSI KWA HABARI ZA MICHEZO PIA UNAWEZA KUTANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU ZAIDI KWA MUDA MREFU ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA +255713 15 33 48

19 November 2014

AZAMFC YAMTAKA KIEMBA KWA MKOPO(SIKIZA SAUTI)




Mabingwa wa soka Tanzania bara Azam FC wametangaza dhamira yao ya kutaka kumsajili kiungo wa klabu ya Simba Amri Ramadhan Kiemba ambae kwa sasa bado anasubiri hatama yake kutoka kwa viongozi wa klabu hiyo ya Msimbazi kufutia tuhuma za kucheza chini ya kiwango katika michezo mitano ya kwanza ya ligi kuu.

Mwenyekiti wa klabu ya Azam FC, Sheikh Said Muhammad Abeid amesema tayari wameshawasilisha ofay a kutaka kumsajili Kiemba baada ya kocha wao kutoka nchini Cameroon Joseph Omog kumpendekeza miongoni mwa wachezajia mbao angependa wasajiliwe katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili..




Hata hivyo mwenyekiti huo wa Azam FC amesema dhumuni lao kwa kiemba ni kumsajili kwa mkataba wa mkopo akitokea Simba na si kumsajili moja kwa moja kama walivyoanza kufanya kwa beki kutoka nchini Ivory Coast Serge Wawa akitokea kwa mabingwa wa soka nchini Sudan El Merekh.





Katika hatua nyingine mwenyekiti wa klabu ya Azam FC, Sheikh Said Muhammad Abeid amekiri kusikitishwa na mwenendo mbovu wa klabu ya Mbeya City ambayo kwa msimu huu ulioshuhudia michezo saba mpaka sasa imeshindwa kufanya makubwa kama ilivyokua msimu uliopita ambapo walicheza ligi kwa mara yao ya kwanza.


17 November 2014

TATIZO LA SOKA LA TANZANIA HATUHESHIMIANI ADOLF RISHAARD (SIKIZA SAUTI)

Katika kuitazama kiundani soka ya Tanzania nimemtafuta mchezaji wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania Adolf Mohamed Rishaard na kocha wa Polisi Moro Kutupatia Tathmini ya soka na msingi mzima wa Uendeshwaji wa soka la Vijana hiki ndicho alichosema Adolf Rishaard

CHEZESHA HAPA 

13 November 2014

MBONA IMEKUWA NONGWA KUHAMIA KARUME(MALINZI SIKIZA SAUTI)





Raisi wa shiriksiho als oka nchini TFF Jamal Malinzi amesema suala la kurejesha ofisi za shiriksiho hilo maeneo ya Karume jijini Dar es salaam kama walivyoshauriwa na FIFA, huenda likachukua muda kutokana na ukarabati ambao unatakiwa kufanywa kwenye ofisi hizo.

Malinzi amesema haoni sababu ya kuharakisha kurejea katika ofisi za zamani za TFF, ili hali FIFA walitoa ahadi ya kusaidia sehemu ya ukarabati wa ofisi hizo, hivyo amewataka wadau wa soka kuwa na subra na jambo hilo japo kuna wengine wanaendelea kulivalia njuga kwa sababu zao binafsi.

Amesema anaamini wapo wanaotamani kuona ofisi za TFF zikirejea Karume kwa malengo mazuri, na pia wapo baadhi ya wadau wa soka nchini ambao wanashinikiza kwa minajili ya kutaka uongozi wake uonekane kama ulikurupuka kuzihamisha ofisi hizo na kuzipeleka kwenye jingo la PPF Tower.



Wakati huo huo Jamal Malinzi akazungumzia sakata la Frank Domayo kusajiliwa na Azam FC, akiwa kwenye kambi ya timu ya taifa ya Tanzania huko mkoani Mbeya miezi sita iliyopita, hatu ambayo ilimfanya kuunda kamati iliyokuwa inaongozwa na Wakili Wilson Ogunde kuchunguza kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina.



12 November 2014

MICHUANO YA MBIO NDEFU INAUA MBIO FUPI (SIKIZA RADIO)




Shirikisho la mchezo wa riadha nchini RT linaandaa mkakati utakaowabana waandaaji michuano ya mbio ndefu ambayo hufanyika kila mwaka, ili kuwawezesha wanariadha wanaokimbia mbio fupi kunufaika na michuano hiyo.

Katibu mkuu wa RT Suleyman Nyambui amesema kwa sasa wamebaini, michuano ya mbio ndefu ambayo hufanyika zaidi ya mara tatu kila mwaka, imekua inashindwa kuwaendeleza vijana wenye malengo la kushindana katika mbio fupi kutokana na mchezo huo kutoshirikishwa kikamilifu.
CHEZA HAPA 
 

Hata hivyo Nyambui amesema wanaamini kuutambulisha mpango huo wa kushirikisha mbio fupi kupirtia michuano yam bio ndefu, kuanzia mwaka 2015 bado haujachelewa kutokana na vijana wengi kuwa katika mikakati ya kukuzwa kupitia michuano mbali mbali ya shule za msingi na sekondari.

lisungu_chisara@yahoo.com

TUTUMIE HABARI YOYOTE YA MICHEZO, BURUDANI TUTAZICHAPISHA

TANGAZA KWA MFUMO HUU


MAHUDHURIO YA WASOMAJI KIMATAIFA

free counters

Followers